Posts

Showing posts from March, 2025

NEMC:Zifahamu fursa zilizopo kwenye taka

Image
  BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limewataka Watanzania kuanza kubadili mtazamo na kuziona taka kama fursa ya kuzirejeleza na kupata bidhaa mbalimbali na kujikomboa kiuchumi. Kauli hiyo imetolewa jana, jijini Dar es Salaam na Meneja Utekelezaji wa Sheria wa baraza hilo, Amina Kibola, wakati akizungumza na waandishi wa habari. Amezungumza wakati akizungumzia siku ya kimataifa ya Siku ya Kimataifa ya Kuondoa Taka, ambayo huadhimishwa kila Machi 30 kila mwaka. Anasema hata kauli mbiu ya mwaka huu, inaweka msisitizo wa kuwa taka si uchafu bali ni malighafi yenye thamani, endapo itasimamiwa na kutumika vyema. Mkurugenzi wa Utekelezaji wa Sheria wa NEMC, Amina Kibola, akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Kibola amesema siku hiyo  ilianzishwa rasmi na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Desemba 2022, ili kukuza mifumo endelevu ya matumizi na uzalishaji na kuongeza uelewa kuhusu udhibiti wa taka. Anasema siku hiyo pia ilianzishwa kwa len...

AINA 6 ZA MABOSI WAKOROFI NA JINSI YA KUKABILIANA NAO....

Image
i. Wanafuatilia Kila Kitu ii. Wanaoamini Katika Mawazo Yao Tu! iii. Wanakuchukia Bila Kujua Sababu iv. Wanaogopa Uwezo Wako v. Wanaokupelekesha vi. Wanaoamini Katika Mawazo Yao Tu! Katika Makala Hii Tutazungumzia Aina ya Nne Ya Mabosi  - Wanaogopa Uwezo Wako  Aina wako mabosi ambao huwa wamejaa hofu kubwa sana ya kupoteza nafasi yao (insecures bosses). Na kwa sababu hiyo kila aliyeko chini yao ambaye anaonekana ni tishio kwa nafasi yao wataanza kumpiga vita kwa nguvu sana.  Mara nyingi sana mabosi wa namna hii utakuta uwezo wao ni mdogo kuliko nafasi waliyonayo.  Mara nyingi unakuta wamepata nafasi hizo kwa mbinu fulani. Kujuana ama kupiga majungu wale ambao walikuwepo kabla yao.  Wakati wowote ule wakiona wewe unaanza kuonesha uwezo mkubwa ambao una hatarisha nafasi yao wataanza kukufanyia visa. Na kukupiga vita ambayo inaweza hata kukuondoa kazini. Kwa ufupi ni kuwa mabosi hawa huwachukia sana watu ambao wenye uwezo mkubwa. Na wanapenda kukaa na watu ambao wan...

Mwalimu Mkuu akamatwa tuhuma za kubaka mwanafunzi Kilosa

Image
Mkuu  wa Shule ya Sekondari Zombo, wilayani Kilosa, Mwalimu Mkame Living Mwaisumo (30), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 16. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro,  SACP Alex Mkama , amesema tukio hilo lilitokea  Machi 19, 2025 , ndani ya ofisi ya mwalimu mkuu, ambako mwanafunzi huyo alikuwa ameagizwa kupeleka mwongozo wa somo (lesson plan). Kamanda Mkama alieleza kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa tukio hilo limetokana na  mmomonyoko wa maadili , huku uchunguzi wa kina ukiendelea ili kukamilisha hatua za kisheria dhidi ya mtuhumiwa. DEREVA ALIYEIBA MAFUTA NA KULICHOMA LORI AKAMATWA Katika tukio lingine, Jeshi la Polisi limemkamata  Abubakar Adam Mwichangwe (29) , mkazi wa  Tabata Kinyerezi, Dar es Salaam , aliyekuwa akisakwa kwa tuhuma za  wizi wa mafuta ya Dizeli lita 35,700  na kuchoma lori alilokuwa akiendesha ili kuonekana kama ajali. Kamanda Mkama amesema kuwa mtuhumiw...

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania anatangaza nafasi za ajira kwa vijana wa kitanzania wenye elimu ya Shahada, Stashahada, Astashahada, Kidato cha sita na Kidato cha nne

Image
  Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania anatangaza nafasi za ajira kwa vijana wa kitanzania wenye elimu ya Shahada, Stashahada, Astashahada, Kidato cha sita na Kidato cha nne >>>>>.>>> BOFYA HAPA KUONA TANGAZO HILO <<<<<<<<

Ulega awasimamisha kazi watumishi mizani waliomnyanyasa dereva Pamela

Image
WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega ametangaza kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi watumishi wa mizani ya barabara nzima ya kuanzia Tunduma (Songwe) hadi Vigwaza (Pwani) waliokuwa zamu Machi 13 mwaka huu kufuatia kuibuka kwa mvutano kati ya watumishi wa mzani wa Vigwaza na dereva wa magari makubwa ya mizigo aliyefahamika kwa jina la Pamela. Katika picha mjongeo iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ilionesha dereva huyo wa magari makubwa ya mizigo ambaye anafanya kazi kwenye kampuni ya Simba Logistics akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari, alisimulia alitokea nchini Congo DRC akiwa amepakia mzigo wa tani 32 na Machi 13 mwaka huu  alipofika mzani wa Vigwaza gari lake lilizuiliwa kwa madai kuwa limezidi uzito. Kufuatia picha hiyo mjongeo, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Ulega ametaja hatua zilizochukuliwa na serikali baada ya yeye kushauriana na menejimenti pamoja na watalaamu mara baada ya Pamela aliyekuwa akiendesha gari lenye namba T137 DLQ na  trela...

Tume huru ya uchaguzi yabaini watu kujiandikisha zaidi ya mara moja

Image
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema imebaini uwepo wa changamoto kwa baadhi ya watu kujiandikisha zaidi ya mara moja katika vituo tofauti wakati wa zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura mkoani Dar es Salaam. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani, huku akibainisha hatua ambazo zinachukuliwa na tume hiyo baada ya zoezi la uandikishaji kukamilika. Amesema baada ya zoezi la uandikishaji kukamilika katika vituo, tume inachakata taarifa za watu wote walioandikishwa kupitia mfumo maalum wa alama za vidole ambao una uwezo wa kuwabaini wapiga kura wote waliojiandikisha zaidi ya mara moja. “Kingine tume hufanya zoezi la kulinganisha sura za watu wote walioko kwenda daftari lengo ni kubaini iwapo kuna waliojiandikisha zaidi ya mara moja. “Pia iwapo itabainika mtu amejiandikisha zaidi ya mara moja, jina na taarifa za mtu huyo, hufutwa na mfumo katika vituo vingine na kubakizwa katika kituo cha mwisho alichojiandikisha ...

Mwalimu, rafikiye wadaiwa kubaka mwanafunzi

Image
  . JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza, linawashikilia Mwalimu wa Shule ya Msingi Bukalu iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na rafiki yake kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake wa kike mwenye umri wa miaka 10. Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Wilbrod Mutafungwa alisema kuwa tukio la mwanafunzi huyo kubakwa na watuhumiwa hao kwa nyakati tofauti tangu mwaka jana, liligundulika mwezi uliopita baada ya kudhoofika kiafya.   Mutafungwa, alisema inadaiwa kuwa watuhumiwa hao walimbaka mwanafunzi huyo kati ya Oktoba 24, mwaka jana hadi Februari 2025 katika nyumba anayoishi rafiki wa mwalimu huyo.  Alisema mwalimu huyo inadaiwa kuwa  alimuita mwanafunzi huyo nyumbani kwake mwezi uliopita kwa kisingizio cha kumfundisha masomo ya ziada na kumbaka.  Kamanda huyo, alisema kwa mujibu wa mama mzazi wa mwanafunzi huyo, Februari 26, mwaka huu, asubuhi alibaini kuwa mtoto huyo afya yake imedhoofika na kuamua kumpeleka hospitali.  Alisema mama huyo alidai baada ya daktari ku...

Trump na Magufuli ni viongozi wa "damu moja" kwa aina yao ya uongozi?

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images  Imetimia miaka minne tangu John Pombe Magufuli, rais wa tano wa Tanzania afariki dunia. Alikuwa mmoja ya viongozi wachache wa Afrika waliovuma sana wakati wa uhai na uongozi wake. Alizungumzwa kila kona kwa namna alivyokuwa akiongoza nchi na watu wake wa Tanzania. Wapo waliomkosoa na wapo waliomuunga mkono kwa namna alivyozungumza, alivyotoa maamuzi na na maagizo, na jinsi alivyochukua hatua kwa masuala mbalimbali, kwananamna fulani ya ufanano kama ilivyo sasa kwa Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye wapo wanaomkoa na wapo wanaomuunga mkono kwa anayoyazungumza na kuyatenda. Baadhi ya watu wanawafananisha kwa kiasi kwa namna wanavyotawala na kuongoza mataifa yao, licha ya tofauti kubwa iliyopo kati ya Tanzania na Marekani kwenye eneo la uchumi, siasa, huduma za kijamii na hata idadi ya watu. Marekani ikiiacha mbali Tanzania kwenye kila eneo. Ingawa viongozi hao waliongoza mataifa yenye historia, tamaduni, uchumi, na siasa tofauti, wote wanasha...