Trump na Magufuli ni viongozi wa "damu moja" kwa aina yao ya uongozi?
Chanzo cha picha, Getty Images Imetimia miaka minne tangu John Pombe Magufuli, rais wa tano wa Tanzania afariki dunia. Alikuwa mmoja ya viongozi wachache wa Afrika waliovuma sana wakati wa uhai na uongozi wake. Alizungumzwa kila kona kwa namna alivyokuwa akiongoza nchi na watu wake wa Tanzania. Wapo waliomkosoa na wapo waliomuunga mkono kwa namna alivyozungumza, alivyotoa maamuzi na na maagizo, na jinsi alivyochukua hatua kwa masuala mbalimbali, kwananamna fulani ya ufanano kama ilivyo sasa kwa Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye wapo wanaomkoa na wapo wanaomuunga mkono kwa anayoyazungumza na kuyatenda. Baadhi ya watu wanawafananisha kwa kiasi kwa namna wanavyotawala na kuongoza mataifa yao, licha ya tofauti kubwa iliyopo kati ya Tanzania na Marekani kwenye eneo la uchumi, siasa, huduma za kijamii na hata idadi ya watu. Marekani ikiiacha mbali Tanzania kwenye kila eneo. Ingawa viongozi hao waliongoza mataifa yenye historia, tamaduni, uchumi, na siasa tofauti, wote wanasha...