Posts

Showing posts from December, 2024

Nawanda afunguka magumu aliyopitia katika kesi ya ulawiti

Image
  ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk. Yahaya Nawanda amezungumza kwa mara nyingine baada ya kushinda kesi ya ulawiti, akisimulia magumu aliyopitia kipindi chote cha kesi hiyo. Dk. Nawanda alieleza hayo juzi wakati wa misa ya kumwombea Rais Samia Suluhu Hassan na kumkumbuka baba mzazi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa iliyofanyika katika mtaa wa Nyakabindi, mjini Bariadi. Alisema kuwa kipindi cha kesi yake kilimfundisha thamani ya kuishi vizuri na watu, akitoa shukrani kwa wananchi wa Simiyu kwa madai walionesha mapenzi makubwa na walimwombea kwa bidii. "Niwashukuru wananchi kwa dua na maombi yenu ambayo mlikuwa mkiniombea wakati ninapitia kipindi kigumu sana ambacho pia nilihitaji uwapo wa Mungu. Kwa hakika Mungu anampa mtihani mtu anayempenda," alisema Dk. Nawanda. Alisema kuwa wakati wowote Mungu hawezi kumpa mtihani mja wake ambao hawezi kuuhimili na kuwa alipewa mtihani huo akijua kuwa atauhimili. "Pia alijua nina watu na watu n...

CHADEMA yasema Hoja hii ya LEMA haitekelezeki,.

Image
  Picha:Mtandao CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimejibu hoja iliyotolewa na Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema kuhusu uteuzi wa mgombea wa nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu ujao. Kupitia akaunti yake ya X, Lema alipendekeza jana kuwa Mkutano Mkuu wa chama hicho utakaofanyika mwezi unaonza kesho, utoke na jina la mgombea urais. Lema pia alipendekeza mkutano utoe mamlaka kwa Kamati Kuu au Baraza Kuu la chama hicho kutafuta mgombea mwenza na kumthibitisha kwa niaba ya mkutano mkuu ili chama kitoke na jina la mgombea sambamba na viongozi wakuu wa chama hicho. "Ingewezekana Mkutano Mkuu wa chama chetu utakaofanyika Januari, utoke na jina la mgombea urais na pia utoe mamlaka kwa Kamati Kuu/Baraza Kuu kutafuta mgombea mwenza na kumthibitisha kwa niaba ya Mkutano Mkuu ili chama kitoke na jina la mgombea sambamba na viongozi wakuu wa chama. "Jambo hili ni muhimu kwa ajili ya 'branding' (kumtangaza kwa lengo kuongeza umaarufu) ya...

Mwanasheria Mkuu mstaafu Jaji Werema afariki dunia, kuzikwa Januari 4 Butiama.

Image
  Aliyekuwa Mwanasheria mkuu wa serikali (AG mstaafu), Jaji Fredrick Werema amefariki dunia katika hospitali ya taifa muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu. Taarifa ya kifo chake imethibitishwa na katibu wa halmashauri ya walei, parokia ya mtakatifu Martha Jimbo kuu la katoliki Dar es salaam, Salome Ntaro. Kwa mujibu wa taarifa Jaji werema amefariki dunia mchana wa tarehe 30, decemba 20245.  Ratiba kamili iliyotolewa na Familia yake ambayo imeeleza kuwa Januari 1,2025 ibada ya kumuombea marehemu itafanyika katika kanisa la mtakatifu Martha, mikocheni jijini Dar es salaam saa 9 alasiri. Aidha, Ijumaa January 3, 2025 baada ya taratibu za kiserikali mwili utaondoka uwanja wa ndege kuelekea Butiama . Chanzo: mwananchi.co.tz

WACHAMBUZI: Wachezaji Wengi wa Ligi Kuu Wana BETI Mechi zao

Image
  Mchambuzi Edga Kibwana amepenyezewa taarifa na mdau kuwa kuna baadhi ya wachezaji wa Ligi kuu wamekuwa wakibet mechi zao hali inayopelekea Ligi kuwa na matukio mengi ya kustaajabisha. Mdau anaziomba mamlaka zinazohusika na Soka kuanza kuchunguza taarifa hizi ili kuwabaini Kutoka kwa Amri Kiemba: “Sisi tunaongea huku tunacheka lakini hali ni mbaya , inawezeka tupo hapa tunasema waamuzi waongezewe ujuzi kumbe wao nyuma wanabet” Katika kuipa uzito hoja yake Kiemba amesema unaweza kushangaa goli ni offside ya wazi lakini mwamuzi anaacha kwa sababu ameweka GG Chanzo:udakuspecial

BONDIA HASSAN MGAYA AFARIKI BAADA YA KUPIGWA "TKO"

Image
  Bondia Hassan Mgaya amefariki dunia baada ya kupigwa TKO katika pambano la raundi sita lililofanyika usiku wa Desemba 28, 2024 ukumbi wa Dunia ndogo Tandale kwa Mtogole jijini Dar es Salaam. Mgaya alicheza pambano hilo ambalo halikua la ubingwa na kupigwa TKO katika raundi ya sita dhidi ya aliyekua mpinzani wake Paulo Elias. Inaelezwa kuwa Mgaya alipigwa na kwenda chini kisha mwamuzi akamhesabia na baada ya mwamuzi kumaliza kuhesabu marehemu akatembea hatua kadhaa hapohapo ulingoni kisha akaanguka na kuzimia. Baada ya kuzimia marehemu akapewa huduma ya kwanza kutoka kwa madakatari waliokuwepo kwenye pambano na akazinduka kisha akapelekwa hospitali ya Sinza kwa ajili ya matibabu, Alipofikishwa hospitali ya Sinza akapatiwa rufaa ya kupelekwa hospital ya Mwananyamala na ndipo umauti ulipomkuta. Kwa upande wake, bondia Cosmas Cheka kutoka chama cha mabondia nchini, amesema kuwa wapo mbioni kuandaa utaratibu wa kumsimamisha muandaaji wa pambano hilo Haji Ngoswe kwa kutoonyesha ushirik...

Lema atoa hadhari CHADEMA kufa, UCHAGUZI WA MWENYEKITI...

Image
  WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikiwa katika maandalizi ya uchaguzi wa viongozi wake ngazi ya taifa, Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema amewaonya wanachama na wafuasi wa chama hicho dhidi ya minyukano inayoendelea. Amesema wanachopaswa kufanya hivi sasa ni kurudi kwenye malengo yao, huku akisisitiza kuwa wakipoteza mwelekeo wa kusudi lao, kuna hatari na chama chao kufa. Alitoa tahadhari hiyo juzi kupitia ukurasa wake wa X (zamani twiter), akisema vita inayoendelea hivi sasa ndani ya wanachama wenyewe kwa wenyewe ni kubwa na ni hatari kwa mustakabali wa chama. Lema ambaye ni Mbunge wa zamani wa Arusha Mjini, alisema kwa hali ilivyo, wanachama wa chama hicho wao kwa wao wanapigana vita vikali kutokana na mgawanyo uliotokana na viongozi wanaowaunga mkono ambao wanagombea nafasi za juu za uongozi kitaifa katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao. "Kwa hali ilivyo sasa, tuna uchungu sisi kwa sisi kuliko tulivyo na uchungu d...

Mrithi wa Kinana kupatikana Januari 2025

Image
 Licha ya kutajwa majina saba ya warithi wa KINANA katika nafasi ya makamu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm. Mrithi atafahamika katika mkutano mkuu maalumu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika tarehe 18 na 19 January 2025. Kwa mujibu wa taarifa za ndani zinadai kuwa lengo la mkutano huo ni kuziba pengo la ABDULRAHMAN KINANA aliyejiuzulu nafasi yake ya makamu mwenyekiti. Chanzo: Mwananchi.co.tz

Hatimaye Ruto aahidi kukomesha utekaji raia

Image
  Rais William Ruto wa Kenya ameahidi kukomesha matukio ya utekaji nyara kufuatia shinikizo la umma baada ya watu kadhaa kutoweka katika miezi ya hivi karibuni ombo vya usalama kwenye taifa hilo la mashariki mwa Afrika vimekuwa vikituhumiwa kwa kuwashikilia makumi ya watu kinyume na sheria tangu yafanyike maandamano ya kuipinga serikali yaliyoandaliwa na vijana katika miezi ya Juni na Julai. Matukio ya hivi karibuni kabisa ya watu kutoweshwa kwa nguvu yamekuwa yakiwahusu vijana wa kiume wanaomkosowa Rais Ruto mitandaoni, huku makundi ya haki za binaadamu yakitupilia mbali madai ya polisi inayokanusha kuhusika na yakitowa wito wa hatua kuchukuliwa kwa haraka. Akizungumza na umati wa watu katika mji wa Homa Bay ulio magharibi mwa Kenya siku ya Ijumaa (Disemba 27), Rais Ruto aliahidi kuchukuwa hatua za kukomesha utekaji nyara huo lakini pia akiwaambia wazazi "wabebe dhamana" ya kuwalea watoto wao. Mahojiano maalumu na Rais William Ruto wa Kenya 12:24 "Tutakomesha utekaji ny...

Taharuki yatanda meli kutitia bandarini

Image
  TAHARUKI ilitanda kwa wakazi wa Mwanza baada ya kuwapo taarifa kuwa meli ya MV. Serengeti, imetitia upande wa nyuma na kuzama ziwani ikiwa imeegeshwa katika bandari ya Mwanza South. Tukio hilo limetokea zikiwa zimepita siku 222 baada ya meli ya MV. Clarias kupinduka na kuanguka majini ikiwa imeegeshwa katika bandari ya Mwanza North. Taarifa za kutitia kwa meli hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 500 na tani 250 za mizigo, zilienea juzi katika mitandao ya kijamii kwamba imezama ikiwa na mizigo. Akizungumza na mwandishi wa habari hii eneo la bandari hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO), Wakili Alphonce Sebukoto, alikiri kutitia kwa meli na kusema haikuwa na safari yoyote tangu mwaka 2016. Sebukoto alisema walipata taarifa kutoka kwa walinzi wa eneo hilo juu ya meli hiyo kutitia na sehemu ya nyuma kuanza kuzama usiku wa kuamkia Desemba 26, majira ya saa 7:00 usiku, hivyo kutuma wataalamu kuanza juhudi za kuiinua. Alisema meli hiyo ni miongoni mwa meli ...

HII HAPA SABABU YA AFISA MTENDAJI KUJINYONGA, NJOMBE

Image
  Sikitu Mwasubila (31) anadaiwa kujinyonga katika mtaa wa Melinze mjini Njombe Disemba 24, 2024 kisa ugumu wa mazingira ya kazi. Inaelezwa kuwa Mwasubila alikuwa Mtendaji wa kijiji cha Mkwayungi mkoani Dodoma ambapo alipata kazi hiyo hivi karibuni na siku kadhaa zilizopita alirudi mjini Njombe anapoishi mume wake kabla ya kujinyonga. Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe ACP. Mahamoud Banga amethibitisha tukio hilo na kuongeza kuwa siku hiyo Marehemu aliandika ujumbe wa kuwaomba radhi ndugu na Mume wake kwa maamuzi aliyoyachukua. >>“(Marehemu) aliacha ujumbe kwamba ndugu zake wamsamehe kwa maamuzi haya ambayo ameyachukua na kwamba mume wake sasa aendelee na maisha na mzazi mwingine ambaye huyo mume wake alizaa naye”amesema Banga Aidha Banga amesema kufuatia operesheni mbalimbali mkoani humo wamefanikiwa kumkamata Regan Sanga (Kihelikopta) akituhumiwa kuongoza genge la wahalifu ambapo mtuhumiwa aliwaongoza Askari na kufanikisha kukamata simu ndogo mpya 25, Simujanja(Smartphone) 9,...

Lema: Maombi yataniongoza kumpata aliye sahihi CHADEMA.

Image
  MWENYEKITI mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema amesema atafanya maombi kwa Mungu kupata upande sahihi wa kuunga mkono katika mvutano wa kumpata mwenyekiti wa chama hicho. Amesema muda si mrefu ataonesha ni upande gani anaounga mkono kati ya Mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Freeman Mbowe na Makamu wake, Tundu Lissu. "Kwa sasa sina timu, pengine siku za usoni ninaweza kujali zaidi juu ya mwelekeo wangu kwa nani ninapenda awe kiongozi mkuu kwenye chama chetu.  "Kwa sasa ninatazama, ninafikiria na kusali, kwa sababu hii position (nafasi) wanayoomba ina umuhimu hata kwangu pia kama mwana-CHADEMA," alisema Lema. Mbowe na Lissu wanagombea nafasi moja ya uenyekiti wa chama hicho taifa na tangu watangaze nia, kumekuwa na mvutano mkubwa mitandaoni kutoka kwa makada na wafuasi wa chama hicho wanaoonekana kugawanyika makundi mawili ya wanaomtaka Mbowe aendelee na wanaomtaka Lissu apokee kijiti hicho. Akizungumza na Nipashe jan...

CLUB YA cs sfaxien YAPEWA ADHABU HIZI NA CAF BAADA YA KUNG'OA VITI

Image
 Club ya cs sfaxien imepewa ADHABU mbili na shitikisho la mpira Africa baada ya Club ya Simba kupeleka malalamiko yake CAF, Kuhusu Vurugu zilizoanzishwa na Waarabu hao baada ya kufungwa Gori dakika za nyongeza na club ya Simba. ADHABU walizopewa cs sfaxien ni zifuatazo:- Kucheza bila mashabiki mechi Yao na Simba na pia mechi Yao na Fc Bravos ADHABU ya kulipia kiasi Cha shilingi za kitanzania sh. Milioni 119 (USD 50,000/=).

TANGAZO LA KUITWA KAZINI (BVR) UBORESHAJI WA DAFTARI TUNDUMA

Image
  Afisa mwandikishaji jimbo la Tunduma anawataarifu waombaji wote wa kazi ya mwandishi msaidizi na mwendeshaji vifaa vya bayometric(BVR ). Aidha waombaji waliochaguliwa wanatakiwa kufika ofisi ya afisa mwandikishajiwa JIMBO la tundumailiyopo mtaa wa Msampania, kata ya Chapwa siku na tarehe watakayoarifiwa. >>>>>>>BOFYA HAPA KUTAZAMA MAJINA YA WALIOITWA KAZINI<<<<<<<<