Posts

Showing posts from October, 2024

UTEUZI:Rais Samia ateua viongozi wapya,,,,

Image
  Dk. Leonard Douglas Akwhilapo  ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU). Dkt. Akwhilapo, ambaye ni Katibu Mkuu Mstaafu, anachukua nafasi ya Prof. Penina Mlama aliyemaliza muda wake. Prof. Zacharia Babuu Mganilwa  ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima. Prof. Mganilwa, Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), anachukua nafasi ya Dk. Naomi Katunzi aliyemaliza muda wake. Dkt. Mwamini Madhebehi Tulli  ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA). Dk. Tulli anahudumu kwa kipindi cha pili. Mhandisi Dk. Richard Joseph Masika  ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji. Dk. Masika anachukua nafasi ya Prof. Henry Mahoo aliyemaliza muda wake. Balozi Salome Thaddaus Sijaona  ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU). Balozi Sijaona ameteuliwa kwa kipindi cha pili. Prof. Joseph Nicolao...

BODI YA MIKOPO WAACHIA MAJINA KWA AWAMU YA NNE

Image
  9,068 WAPANGIWA MIKOPO YA TZS 27.5 BILIONI AWAMU YA NNE Dirisha la Rufaa kufunguliwa Novemba 4 -11, 2024 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu leo ( Jumanne, Oktoba 29, 2024)  imetangaza Awamu ya Nne  (Batch Four)  yenye wanafunzi  9,068  wa shahada ya awali (Bachelor Degrees) na stashahda (Diploma) waliopangiwa mikopo yenye thamani  TZS 27.52 bilioni  kwa mwaka wa masomo  2024/2025. Wanafunzi  4,400  wa mwaka wa kwanza waliodahiliwa katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo nchini kwa ajili ya masomo ya shahada za awali na wamepangiwa mikopo yenye thamani ya  TZS 13.74  bilioni . Awamu hii pia imewajumuisha wanafunzi  2,646  wa shahada ya awali wanaoendelea na masomo ambao wamepangiwa mikopo kwa mara ya kwanza  (first-time continuing)  yenye thamani ya  TZS  8.37 bilioni. Mikopo kwa Stashahada Katika awamu ya nne iliyotangazwa leo, wamo pia wanafunzi wapya  2,022  w...

HAYA HAPA MATOKEO YA DARASA LA SABA

Image
  Leo tarehe 29/10/2024 Baraza la mitihani limetangaza matokeo ya Darasa la saba Kwa mwaka 2024 Jumla ya watahiniwa 974,229 Sawa na 80.87%, watahiniwa wenye matokeo wamefaulu na kumaliza Elimu ya Msingi 2024, hivyo ufaulu wa jumla umeongezeka kwa 0.29%, Kati ya watahiniwa hao wavulana ni 449,057 Sawa na 81.85% na wasichana ni 525,172 Sawa na 80.05%, hivyo ufaulu wa wasichana umeshuka kwa 0.53% na ufaulu wa wavulana umeongezeka kwa 1.26%”, Dk.Said Mohamed, Katibu Mtendaji NECTA <<<<<<<BOFYA HAPA KUTAZAMA>>>>>>>>

Chino Kid: Mimi na Marioo Tumesaidiana, Alinikuta Tayari Mimi ni Mkubwa Katika Game

Image
  Msanii Bora Chipukizi kwenye Tuzo za #TMA, @chino_kidd7 amefunguka kuhusu kuacha kumtaja Staa wa muziki @marioo_tz kama moja ya watu wenye mchango kwenye safari yake ya Music. . Akizungumza kwenye #Whatspoppin ya #Cloudsfm #Chino amesema kuwa…. “Nilikuwa na furaha sana ile siku ndio maana sikumaliza maneno yote kuna baadhi ya maneno nilikosea kwa furaha, Kuna watu wengi sikuwataja kama kina @s2kizzy lakini sipendi kutengenezewa stori mimi ni kijana ninaepambana na nina mchango kwa wasanii kibao sio lazima niwe naongea” “Ukizingatia @marioo_tz mimi ni mkubwa kuliko yeye nimezaliwa 1995 lakini tulianza kazi tukiwa tunapambana hatuna kitu Kwahyo wote tumesaidiana kwahyo #Marioo anapaswa kunishukuru na Mimi” “Nimekutana na #Marioo mimi tayari ni Dancer wa #RichMavoko najulikana nmewahi kucheza mpaka #WCB, #RichMavoko ndio amefanya watu wanijue “

Huyu Ndio Bondia KANYABOYA Kutoka Burudi Aliyeleta Msemo wa Kanya Boya Tanzania Kutokana na Vitendo vyake

Image
  Kanya Boya ni bondia wa ngumi za kulipwa kutoka Burundi. Bondia huyu Felix Kanyaboya kati ya Miaka ya 1986 / 1987 alikuja kucheza Tanzania , Alikuwa anafikia Hotel za Kariakoo. Bondia huyu alikuwa na Mikwara mingi saana na siku ya Mechi anatoka Hotelini Kariakoo anatembea kwa Miguu akiwa kavalia kabisa Gloves , ring bout, Gum shield, anapiga shadow box njia nzima na watu wanamshangilia mpaka Railways Club Gerezani. Akipanda Ulingoni Round zake 2 tu kapigwa KO mbaya na akina Habibu Kinyogoli, na Omary Yazidu. Ndipo Jina lake likavuma kama *KANYABOYA* NI KUMBUKUMBU TU Kutoka Maktaba.

Mwigizaji na Mchekeshaji Mkongwe Nchini PEMBE Afariki Dunia

Image
  Mwigizaji na Mchekeshaji Mkongwe Nchini PEMBE Afariki Dunia Mwigizaji na Mchekeshaji Mkongwe Nchini Tanzania, Mzee Yusuph Kaimu maarufu Pembe amefariki dunia jioni ya leo October 20,2024 katika Hospitali ya Temeke Jijini Dar es salaam alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu. Baadhi ya Waigizaji akiwemo Vicent Kigosi (Ray) na Mau Fundi wametoa taarifa za msiba huo na kusema taratibu za mazishi zitatolewa baadaye, Katibu wa Chama cha Waigizaji Kinondoni, Jafari Makatu ambaye amethibitisha na kusema “Alikuwa anaumwa alilazwa Temeke Hospital, amefariki kama saa moja iliyopita, alilazwa kama siku tatu nne, na tulikuwa tumepanga kwenda kumuona Kesho baada ya kuambiwa anaumwa” Tunduma zone tunatoa pole kwa Waigizaji, Wachekeshaji, Ndugu, Jamaa na Marafiki na wengine wote walioguswa na msiba huu, Mungu amlaze pema Ndugu yetu Pembe. Chanzo:udaku special 

Mahakama yasitisha kuondolewa kwa Gachagua ofisini

Image
  Mahakama kuu imesitisha utekelezwaji wa azimio la Seneti la kuidhinisha mashtaka ya kumuondoa madarakani Rigathi Gachagua. Uamuzi huo umetolewa muda mfupi tu baada ya Bunge la Kitaifa kuafiki uteuzi wa Kithure Kindiki kuwa Naibu wa Rais baada ya Rais William Ruto kuwasilisha jina lake kwenye bunge hilo. Hapo jana Maseneta nchini humo waliidhinisha mashtaka 5 kati ya 11 dhidi ya Gachagua na kumuondoa ofisini. Gachagua alikosa kufika mbele ya maseneta kujitetea baada ya mawakili wake kusema alipatwa na ''maumivu makali ya kifua'' na kulazimika kulazwa hospitalini. Uamuzi uliotolewa na Jaji E.C. Mwita umezuia kutekelezwa kwa azimio hilo la seneti na pia kuzuia rais kumteua mtu kuichukua nafasi hiyo hadi tarehe 24 mwezi huu hadi kesi hiyo sikilizwe na jopo la majaji watakaoteuliwa na Jaji Mkuu Martha Koome. Hata hivyo tayari rais amependekeza jina la Kithure Kindiki kuichukua nafasi ya Gachagua na bunge la taifa kuafiki uteuzi wake.

Kithure Kindiki sasa ndiye Naibu Rais mteule

Image
  Bunge la Kitaifa limeafiki uteuzi wa Profesa Kithure Kindiki kuwa Naibu Rais mteule wa Kenya baada ya jina lake kuwasilishwa na Rais William Ruto. Wabunge 236 walipiga kura ya 'Ndiyo' kuafiki uteuzi wa Kindiki . Jina lake sasa litawekwa katika gazeti rasmi la serikali na kisha kuapishwa kuanza kuhudumu kama Naibu Rais . Katiba inasema pindi rais anapowasilisha uteuzi kwenye Bunge, wabunge watapiga kura ya kulikataa au kuliidhinisha jina hilo. Pia hakuna sharti la kura ya thuluthi mbili. “Prof. Kindiki, ambaye kwa sasa anahudumu kama Waziri wa Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa, atahitaji idhini kutoka kwa Bunge la Kitaifa kabla ya kushika nafasi ya Naibu Rais. Bunge lazima lipigie kura uteuzi ndani ya siku 60 baada ya kupokea jina hilo. Baada ya kuidhinishwa, mteule atateuliwa rasmi na Rais kuwa naibu wake. Ingawa Katiba haijaweka bayana muda wa uteuzi huu, unatarajiwa kutokea mara baada ya kuidhinishwa na Bunge.

Maseneta nchini Kenya wamuondoa Naibu wa rais Gachagua.

Image
  Maseneta wa Kenya wamepiga kura ya kumuondoa Naibu Rais Rigathi Gachagua ofisini licha ya kushindwa kutoa ushahidi wake katika kesi ya kumuondoa madarakani baada ya wakili wake kusema kuwa amepelekwa hospitalini. Katika moja ya siku za kushangaza katika historia ya hivi majuzi ya kisiasa nchini Kenya, Gachagua alipaswa kufika katika Seneti baada ya chakula cha mchana kujitetea, siku moja baada ya kukanusha mashtaka 11. Hata hivyo, Gachagua, almaarufu Riggy G, hakufika na wakili wake akaomba kuahirishwa akisema mteja wake alikuwa akisumbuliwa na 'maumivu ya kifua' na alikuwa akitibiwa na madaktari katika Hospitali ya The Karen. Hata hivyo baada ya muda wa saa mbili kutoka saa tisa mchana hadi saa kumi na moja jioni Gachagua hakuweza kufika bungeni  Maseneta wa Kenya wamepiga kura ya kumuondoa Naibu Rais Rigathi Gachagua ofisini licha ya kushindwa kutoa ushahidi wake katika kesi ya kumuondoa madarakani baada ya wakili wake kusema kuwa amepelekwa hospitalini. Katika moja ya sik...

KATIBU CCM(BALOZI NCHIMBI) AMJIBU KATIBU CHADEMA KUHUSU UCHAGUZI

Image
  CHAMA Cha Mapinduzi CCM kimejibu kauli iliyotolewa juzi na Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika aliyoilaumu TAMISEMI na CCM kwamba hawafanyi jitihada za kutosha kuhamasisha watu kujitokeza kujiandikisha kwenye dafatari la wakazi katika uchaguzi wa serikali za mtaa. Mnyika aliongeza hata Halmashauri zilizopewa jukumu la kusimamia uandikishaji huo kwa muujibu wa mwongozo na kanuni za Serikali ya Mitaa hazijafanya hivyo. Akijibu hoja hiyo, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi akiwa ziarani Malampaka Maswa mkoani Simiyu  amesema ameona katika mitandao ya kijamii kiongozi mmoja wa upinzani bila kimtaja jina analalamika kuhusu suala hilo. "Kiongozi huyo amesema CCM na TAMISEMI kwa makusudi hawahamasishi watu kujiandikisha, hawahamasishi watu kupiga kura nikacheka nikasema hawa wenzetu hawa. Sisi mikoa yote 18 tunazunguka tunahamasisha si mnatusikia huko kwenye redio. "Tunahamasisha watu wajiandikishe, watu wapige ku...

BODI YA MIKOPO YATOA ORODHA YA AWAMU YA PILI

Image
  Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo Jumatano (Oktoba 09, 2024) imetangaza awamu ya pili ya orodha ya wanafunzi wenye sifa waliopangiwa mikopo na ruzuku kwa ajili ya mwaka wa masomo   2024/2025. Makundi ya walionufaika katika Awamu ya Pili Orodha iliyotangazwa leo inajumuisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliodahiliwa katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu na vyuo vya kati waliopangiwa mikopo kwa ajili ya Shahada ya awali ( 30,311)  yenye thamani ya  TZS 93.7 bilioni.  Orodha ya awamu ya pili inafanya idadi ya jumla ya wanafunzi  51,645  waliopangiwa mikopo katika awamu ya kwanza na awamu ya pili kwa ajili ya kugharimia masomo yao ya shahada ya awali ikiwa na thamani ya  TZS 163.8 bilioni.  Kati ya wanafunzi hao, wanafunzi wa kike ni  22,216  (sawa na  43% ) na wa kiume  29,429  (sawa na  57% ) Awamu hii ya pii inajumuisha pia mikopo ya Stashahada (Diploma) kwa wanafunzi wapatao  2,157...

CHADEMA yaweka nguvu uchaguzi Serikali za Mitaa

Image
Home Habari Biashara Michezo Burudani Makala Safu Maoni Maktaba EDITIONS The Guardian Nipashe Nipashe Jumapil IKIWA zimebaki siku mbili kuanza kwa uandikishwaji wa wananchi Daftari la Wakazi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, mwaka huu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, alisema ni muhimu kwa wananchi wote wenye sifa kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari hilo Oktoba 11 hadi 20 ili waitumie vizuri haki yao ya kuchagua viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji. Alisema CHADEMA kimeamua kuongeza kasi ya uhamasishaji kwa sababu wameona suala hilo halijapewa uzito mkubwa wakati siku za kujiandikisha zinakaribia. “Nimewaita kupitia kwenu kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa ya kupiga kura ambao ni wakazi wa mtaa wenye umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, kuanzia Oktoba 11 mpaka 20, kote...

Bashungwa ataka watumishi wa umma kuacha urasimu

Image
  Home Habari Biashara Michezo Burudani Makala Safu Maoni Maktaba EDITIONS The Guardian Nipashe Nipashe Jumapil Picha: Julieth Mkireri WAZIRI wa Ujenzi Innocent Bashungwa. WAZIRI wa Ujenzi Innocent Bashungwa amesema watumishi wa umma wanatakiwa kuacha tabia ya urasimu kazini mambo ambayo yanachelewesha uwekezaji. A mesema Mkoa wa Pwani ni eneo lenye fursa ya uwekezaji hivyo mambo hayo yasipofanywa na watumishi yanawavutia wawekezaji kuwekeza kwa wingi . Bashungwa ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi na viongozi mbalimbali wa mkoa huo walioshiriki kikao kabla ya kuanza ziara ya kikazi anayoifanya katika Mkoa wa Pwani akianzia Wilaya ya Kibaha. Akizungumza na wananchi katika maeneo tofauti wa Wilaya ya Kibaha amesema Serikali inaendelea na maboresho kwenye barabara kwa kuzijenga katika kiwango cha changarawe na lami kwa kutenga fedha kupitia bajeti zake. Pia Bashungwa amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Pwani Baraka Mwambage kutengeneza kwa kiwango...