Kithure Kindiki sasa ndiye Naibu Rais mteule
Bunge la Kitaifa limeafiki uteuzi wa Profesa Kithure Kindiki kuwa Naibu Rais mteule wa Kenya baada ya jina lake kuwasilishwa na Rais William Ruto. Wabunge 236 walipiga kura ya 'Ndiyo' kuafiki uteuzi wa Kindiki .
Jina lake sasa litawekwa katika gazeti rasmi la serikali na kisha kuapishwa kuanza kuhudumu kama Naibu Rais .
Katiba inasema pindi rais anapowasilisha uteuzi kwenye Bunge, wabunge watapiga kura ya kulikataa au kuliidhinisha jina hilo. Pia hakuna sharti la kura ya thuluthi mbili.
“Prof. Kindiki, ambaye kwa sasa anahudumu kama Waziri wa Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa, atahitaji idhini kutoka kwa Bunge la Kitaifa kabla ya kushika nafasi ya Naibu Rais. Bunge lazima lipigie kura uteuzi ndani ya siku 60 baada ya kupokea jina hilo.
Baada ya kuidhinishwa, mteule atateuliwa rasmi na Rais kuwa naibu wake. Ingawa Katiba haijaweka bayana muda wa uteuzi huu, unatarajiwa kutokea mara baada ya kuidhinishwa na Bunge.
Comments
Post a Comment