Posts

HUU HAPA ๐”๐’๐‡๐”๐‰๐€๐€ ๐–๐€ ๐Œ๐‚๐‡๐„๐†๐„๐‘๐–๐€ ๐Š๐€๐“๐ˆ๐Š๐€ ๐Š๐”๐ˆ๐Œ๐€๐‘๐ˆ๐’๐‡๐€ ๐“๐€๐€๐’๐ˆ๐’๐ˆ ๐๐€ ๐Š๐”๐’๐ˆ๐Œ๐€๐Œ๐ˆ๐€ ๐Œ๐€๐„๐๐ƒ๐„๐‹๐„๐Ž ๐๐‚๐‡๐ˆ๐๐ˆ ๐Š๐”๐๐ˆ๐“๐ˆ๐€ ๐“๐€๐Œ๐ˆ๐’๐„๐Œ๐ˆ

Image
  Katika mwaka 2024, Mohamed Mchegerwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ameonyesha uongozi wa kipekee uliojikita katika misingi ya haki, uwazi, na maendeleo ya wananchi. Kupitia juhudi zake, amefanikisha mambo makubwa ambayo yameacha alama isiyofutika katika historia ya utawala na maendeleo ya nchi yetu. ๐—ž๐˜‚๐—ฟ๐—ฒ๐—ท๐—ฒ๐˜€๐—ต๐—ฎ ๐— ๐—ถ๐—ธ๐—ผ๐—ฝ๐—ผ ๐˜†๐—ฎ ๐—›๐—ฎ๐—น๐—บ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐—ฎ๐˜‚๐—ฟ๐—ถ Moja ya mafanikio makubwa ya Waziri Mchegerwa ni kuhakikisha mikopo ya halmashauri imerejea na kuanza kufanya kazi kwa ufanisi. Mikopo hii imekuwa nyenzo muhimu katika kuinua uchumi wa wananchi hasa kupitia vikundi vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu. Kwa kuweka mifumo imara ya usimamizi wa fedha, Waziri Mchegerwa amehakikisha kuwa mikopo inatolewa kwa uwazi na kufikia walengwa kwa wakati muafaka. Hii imeongeza imani ya wananchi kwa halmashauri na kuimarisha mshikamano kati ya serikali na wananchi. ๐—จ๐˜€๐—ถ๐—บ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐˜‡๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐— ๐—ถ๐—ฟ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐——๐— ๐——๐—ฃ ๐—ฃ๐—ต๐—ฎ๐˜€๐—ฒ ๐Ÿฎ ๐—ป๐—ฎ ๐—ง...

Christina Shusho Amtetea Martha Mwaipaja Jukwaani, Alichofanya Upendo Nkone Utapenda

Image
   Christina Shusho Amtetea Martha Mwaipaja Jukwaani, Alichofanya Upendo Nkone Utapenda. CHANZO.:UDAKUSPECIALLY

Makubwa: Joan Anayedai ni Mtoto wa Martha Mwaipaja Aingia Live na Kuongea Haya, Wengi Wamshangaa (VIDEO)

Image
 Makubwa: Joan Anayedai ni Mtoto wa Martha Mwaipaja Aingia Live na Kuongea Haya, Wengi Wamshangaa.

Jean Baleke Apotea Kusiko Julikana, Mazoezini na Yanga Haendi Tena...

Image
  MSHAMBULIAJI wa Yanga Jean Baleke amejiweka karibu na mlango mgumu wa kutokea baada ya kukacha mazoezi ya timu hiyo. Baleke hajaonekana ndani ya kambi ya Yanga kwa zaidi ya wiki moja akikosa ratiba zote za mazoezi ya timu hiyo huku pia hata uwanjani akikosekana. . Mshambuliaji huyo alikuwa katika msafara wa Yanga ikiifuata MC Alger ya Algeria kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika lakini hakukaa hata benchini. Baada ya hapo Baleke ambaye anaichezea Yanga kwa mkopo hajaonekana tena kwenye kambi ya Yanga. CHANZO: https://www.udakuspecially.com/

MWENYEKITI BAWACHA PWANI: Naona umuhimu wa ukomo wa uongozi hapo mbeleni

Image
  MWENYEKITI wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA), Kanda ya Pwani, Rose MoshI, amesema pamoja na haki ya kila mwanachama kumuunga mkono kiongozi ambaye wanaona anafaa ndani ya chama, hapo mbeleni kunapaswa kuwapo ukomo wa uongozi. Amesema kwa miaka ijayo, ipo haja ya kuwapo ukomo wa uongozi ndani ya chama na katiba kuweka wazi, ili kutoa fursa kwa wanachama wengine kuonesha maono yao kiuongozi. Rose amesema hayo leo, akihojiwa na redioni Clouds fm, kuhusu mtazamo wake binafsi wa hatua ya Freeman Mbowe, kuonesha nia ya kuwania tena nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Amesema ameungana na wanawake wengine ambao wanaona ni vyema kumuunga mkono Mbowe, kushika nafasi hiyo, kwa kuwa kwa wakati huu kulingana na mwenendo wa kisiasa nchini, Mbowe anafaa.

RC Simiyu awaongoza wananchi kumuombea Rais Samia

Image
  MKUU wa Mkoa wa Simiyu Kenani Kihongosi amewaongoza viongozi na wananchi mbalimbali mkoani humo kumwombea Rais Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuendelea kuwa imara katika kuliongoza taifa. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya kiongozi huyo, maombi hayo yamefanyika leo mkoani Simiyu sambamba na matembezi, yaliyolenga kuhamasisha udumishaji wa amani na utulivu kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka. "Mbali na kumuombea Rais, maelfu ya wananchi walitumia nafasi hiyo kuliombea taifa kuvuka salama mwaka 2024 na kuingia 2025 likiwa na umoja, wenye amani na mshikamano," imesema sehemu ya taarifa hiyo. 1 2 3

Waziri Mchengerwa Acharuka, Aipinga Vikali Kauli ya Paul Makonda

Image
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, maarufu kama "Mtu Kazi," amejitokeza hadharani na kulaani vikali kauli tata iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha. Mkuu huyo wa mkoa alikuwa amepongeza tukio la kusikitisha ambapo wananchi walimvamia na kumtembeza diwani kwenye matope. Waziri Mchengerwa amesisitiza kuwa matendo ya aina hiyo si maagizo ya serikali na kwamba viongozi hawapaswi kuhamasisha wananchi kuchukua sheria mikononi. Akizungumza leo katika mkutano na waandishi wa habari, Mchengerwa alisema, "Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina sera ya kuchochea vurugu au kutoa adhabu nje ya mfumo wa kisheria. Kauli kama hizi si tu zinavuruga utawala wa sheria, bali pia zinachochea ghasia zisizo za lazima." Kauli ya Mkuu wa Mkoa imeibua hasira na masikitiko miongoni mwa wananchi, huku wengi wakishangazwa na uungwaji mkono wa matendo yasiyo ya kistaarabu. Tukio hilo, ambalo lilisambaa mitandaoni, limea...