RC Simiyu awaongoza wananchi kumuombea Rais Samia

 


MKUU wa Mkoa wa Simiyu Kenani Kihongosi amewaongoza viongozi na wananchi mbalimbali mkoani humo kumwombea Rais Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuendelea kuwa imara katika kuliongoza taifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya kiongozi huyo, maombi hayo yamefanyika leo mkoani Simiyu sambamba na matembezi, yaliyolenga kuhamasisha udumishaji wa amani na utulivu kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka.

"Mbali na kumuombea Rais, maelfu ya wananchi walitumia nafasi hiyo kuliombea taifa kuvuka salama mwaka 2024 na kuingia 2025 likiwa na umoja, wenye amani na mshikamano," imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

NEMC:Zifahamu fursa zilizopo kwenye taka

APPLICATIONS hizi HAPA haziruhusiwi kutoa mikopo mtandaoni

Geofrey Kiliba, rais mpya wa TAHLISO