Posts

Showing posts from November, 2024

TAIFA STARS INAWEZA KUONDOLEWA KUSHIRIKI MICHUANO YA AFCON 2025,,, KWA SABABU HIZI HAPA....?

Image
  Huenda timu ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS ikakumbwa na adhabu ya kuondolewa katika michuano ya AFCON 2025, Kwa kosa la kumuingiza mchezaji IBRAIMU AME akiwa amevalia Jezi nambari  ''26'' lakini katika orodha iliyowasilishwa CAF hakunamchezaji mwenye jezi nambari ''26''  Kama ambavyo Guinea walivyoripoti  Shirikisho la mpira CAF. TUENDELEE KUFUATILIA  Tundumazone.blogspot.c0m

APPLICATIONS hizi HAPA haziruhusiwi kutoa mikopo mtandaoni

Image
  ENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetangaza application 69 ambazo haziruhusiwi kutoa huduma za mikopo mtandaoni kwa kuwa hazina kibali na haziruhusiwi kuendesha shughuli hizo, huku ikiitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuzifungia. Hatua hii inakuja mwezi mmoja tangu Nipashe iibue kero iliyopo kwenye mikopo mtandaoni, huku kasi ya udhalilishaji na utoaji riba kubwa ambao hauna utaratibu wa kisheria hadi BoT ilivyotoa mwongozo kwa watoa huduma hao na kuwataka wajisajili. Licha ya kupewa siku 14, walijitokeza waombaji 16 na kati yake 14 pekee walikidhi vigezo, huku BoT ikichukua hatua kali kwa Microfinance ambazo zilianzisha Apps na kutoa mikopo mtandaoni.  Taarifa kwa umma iliyotolewa jana na Gavana wa BoT, Emmanuel Tutuba: “Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuufahamisha umma kuwa imebaini kuwepo kwa Majukwaa na Programu Tumizi ‘Applications” zinazojihusisha na utoaji wa mikopo kidijitali bila ya kuwa na leseni na idhini kutoka Benki Kuu ya Tanzania.” Kupitia taarifa hii, Ben...

Rais Samia: Tukio Hili Linaashiria Mapungufu ya Kiutendaji na Uwajibikaji

Image
  “Basi wito wangu kila mmoja atimize wajibu wake kikamilifu, ukiangalia jengo hili lilivyojengwa bila shaka lilipata vibali kutoka taasisi ya serikali halmashauri. “Kibali jambo moja usimamizi jambo jingine jengo halikutazamwa ubora wake wakati wa ujenzi, niwaombe watu wote tunaohusika kwenye mambo haya Serikali Kuu, Halmashauri, viongozi wa serikali za mitaa asasi za kiaraia na wananchi wote kwa ujumla tuseme kwa pamoja kwamba matukio ya aina hii yasijirudie kwasabu tukio hili ni huzuni kubwa sana kwa taifa letu” Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi alipotembelea katika eneo lililoporomoka jengo la ghorofa Kariakoo, Dar es Salaam.

Yanga Kumsajili Mshambuliaji Huyu Kutoka Uganda...Noma na Nusu

Image
  YANGA imeanza mikakati ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji katika dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa Desemba 15 mwaka huu ambapo jina la mshambuliaji Bayo Aziz Fahad ndio kipaumbele chao cha kwanza. Bayo mwenye umri wa miaka 26, inaripotiwa kuwa ameshafanya mazungmzo na kumalizana na vigogo wa Yanga ambapo wamefikia pazuri huku kilichobaki kwa mchezaji huyo ni kusubiri dirisha dogo ili ajiunge nayo. Uwezo wa kufunga na kupiga pasi za mwisho ambao Bayo amekuwa nao unaonekana kuiridhisha Yanga ambayo ujio wa mshambuliaji huyo utasaidia safu yake ya ushambuliaji lakini pia kuwaongezea ushindani chanya washambuliaji waliopo kikosini ambao wanaonekana bado wanajitafuta. Kwa sasa, Bayo ni mchezaji huru baada ya kuachana na MFK Vyskov inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Czech ambayo aliichezea mechi 42 na kuifungia mabao manane. Kabla ya kujiunga na Vyskov, Bayo aliitumikia Ashdod inayoshiriki Ligi Kuu ya Israel ambako katika mechi 41 alizoichezea, alifunga mabao manane...

WARAKA WA ELIMU NA.02 WA MWAKA 2024 KUHUSU KALENDA YA MIHULA YA MASOMO KWA SHULE ZA AWALI NA MSINGI NA SEKONDARI MWAKA 2025

Image
WARAKA WA ELIMU NA.02 WA MWAKA 2024 KUHUSU KALENDA YA MIHULA YA MASOMO KWA SHULE ZA AWALI NA MSINGI NA SEKONDARI MWAKA 2025 <<<<<<BOFYA HAPA KUSOMA WARAKA>>>>>

HATIMAYE Yanga Wamtangaza Kocha Huyu Mpya

Image
  Yanga SC wamemtangaza rasmi  Sead Ramovic  (45) Raia wa Ujerumani kuwa Kocha wao Mkuu akija kuchukua mikoba ya Miguel Gamond ambaye amefutwa kazi na Yanga SC saa chache zilizopita. Sead anajiunga na Yanga akitokea TS Galaxy ya Afrika Kusini aliyodumu nayo kwa miaka mitatu 2021-2024 kabla ya kujiunga na Yanga SC ya Tanzania. Sead hana uzoefu sana wa soka la Afrika lakini wasifu wake unaonesha amewahi kucheza soka katika vilabu vikubwa vya Ligi Kuu Ujerumani kama VFL Wolfsburg na Borussia Mongladbach.

Mambo Matano Yanayoivuruga Klabu ya Yanga kwa Sasa.

Image
  Mambo yameendelea kuwa magumu klabu ya Yanga baada ya kukumbwa na misukosuko mingi ndani ya muda mfupi. Leo tarehe 15 Novemba Yanga wametangaza kuachana na waliokuwa makocha wa klabu hiyo ambao ni Miguel Gamondi kocha mkuu na Mousa Ndauw kocha msaidizi. Hizi ni nyakati mbaya kwa klabu hiyo na kuna uwezekano likawa anguko la klabu hiyo katika mbio za kutetea ubingwa wa ligi ya NBC na kombe la CRDB. Nimekuandalia mambo matano yanayoivuruga klabu ya Yanga kwa sasa. 1.Kufungwa na Azam pamoja na Tabora United Klabu ya Yanga ilianza vyema msimu wa 2024/25 kwa kushinda mechi 8 za awali na kuwa kinara kwenye msimamo wa ligi wakijikusanyia alama 24 na katika mechi hizo walifunga mabao 14.Mchezo dhidi ya Azam walipoteza kwa bao 1-0 na mchezo dhidi ya Tabora United walipoteza kwa mabao 3-1.Kupoteza michezo hiyo kuliibua gumzo klabuni hapo na hoja ya kumfukuza kocha Gamondi ilianza kuchochewa moto na hatimaye leo ametimuliwa. Kama umetazama michezo hii miwili ambayo Yanga wamepoteza utagundu...

Taarifa ya Ghorofa Kuanguka Kariakoo, Waziri Mkuu Athibitisha Mmoja Kufariki...

Image
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amethibitisha kutokea kwa kifo cha mtu mmoja na wengine 28 kuokolewa wakiwa wamejeruhiwa katika ajali ya kuporomoka kwa ghorofa iliyotokea asubuhi ya leo, Novemba 16 Kariakoo jijini Dar es Salaam. Akizungumza kwenye eneo la ajali, Waziri Mkuu amesema serikali kupitia kwa vikosi vya uokoaji itahakikisha shughuli hiyo inafanyika mpaka watu wote waliokuwepo kwenye jengo hilo wakati wa ajali wanathibitika iwapo wako hai au wamefariki. Nacho kikosi cha zimamoto na uokoaji kimesema kuwa kinaendelea na juhudi za kuwaokoa watu walionaswa kwenye vifusi ikiwa ni pamoja na kuwapelekea hewa ya oksijeni kupitia mipira maalumu ili kuwasaidia kupata hewa safi wakisubiri uokozi. Shughuli ya uokoaji inaendelea katika kifusi cha ghorofa hilo lililokuw akatika makutano ya mtaa wa Kongo na Mchikichi.

Mwenyekiti CHADEMA Singida abwagwa

Image
  MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Singida, Jackson Jingu, ameshindwa kutetea nafasi yake baada ya kushindwa vibaya na Diwani wa Kata ya Ntuntu wilayani Ikungi, Omari Mohamed Toto. Kutokana na hilo, Jingu ametangaza Uchaguzi Mkuu 2025 atawania ubunge katika Jimbo la Singida Magharibi. Katika uchaguzi huo uliofanyika juzi mjini Singida ambao pia, ulihudhuriwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, Jingu aliambulia kura 30 dhidi ya mpinzani wake, Toto aliyeibuka kidedea kwa kupata kura 52, huku nafasi ya tatu ikishikwa na Wilson Luta aliyepata kura tano. Msimamizi wa uchaguzi huo Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Patrick Ole Sosopi, akitangaza matokeo hayo alisema nafasi ya Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Singida, aliyeshinda ni Samweli Maro kwa kupata kura 58 na hivyo kufanikiwa kutetea nafasi yake hiyo. Alisema nafasi Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Mkoa wa Singida, ilichukuliwa na Joseph Salum huku uchaguzi wa nafasi Katib...