Kitumbua cha Ruto na Gachagua kinavyoingia mchanga na kuzua joto la kisiasa Kenya

 

th

Chanzo cha picha,RUTO CAMPAIGN

  • Author,

Miaka miwili tu baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya uliowaingiza madarakani Rais William Ruto na naibu wake Rigathi Gachagua, yaonekana kipindi cha fungate kimefika tamati.

Wiki za hivi karibuni katika siasa za Kenya zimeshuhudia kile kinachoweza kuitwa 'sarakasi' za siasa za Kenya ila inakuwa wazi kwamba kila mambo yanavyobadilika, ndivyo yanavyosalia yalivyokuwa -na hasa katika siasa za taifa hilo la Afrika mashariki.

Naibu wa rais Gachagua sasa anakabiliwa na tishio la kutimuliwa mamlakani kupitia hoja itakayowasilishwa bungeni na washirika wa Rais William Ruto. Katika upande mmoja wa malumbano hayo ni rais na viongozi wa chama tawala cha United Democratic Alliance (UDA) wanaoumuunga mkono na katika upande wa pili ni naibu wake na viongozi ambao wamesimama naye.

Hatua ya hivi punde inayoashiria kuzorota kwa uhusiano kati ya wawili hao ni ile ya Waziri wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki kutangaza kwamba serikali itawafungulia mashtaka viongozi kadhaa wanaodaiwa kupanga na kufadhili maandamano ya vijana yaliyotikisa serikali miezi ya Juni na Julai. Wanaohusishwa na njama hizo ni washirika wa Naibu wa Rais.

Ufichuzi huo unajiri wiki moja tu baada ya Gachagua kufichua 'mateso' aliyosema ameyapitia katika muda wa mwaka mmoja uliopita alipohojiwa katika kituo cha runinga na Citizen.

Katika mahojiano hayo Gachagua alitoa kauli ambazo zimewaghadhabisha sana washirika wa rais Ruto na kuwafanya kujizidisha harakati zao za kutaka kumuondoa mamlakani. Je, ngoma hii itaishia wapi?

Comments

Popular posts from this blog

WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2025 MAJINA HAYA HAPA.

TAZAMA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024.