Watu 17 wauawa katika ufyatulianaji risasi Afrika Kusini

 




Watu kumi na saba wakiwemo wanawake 15 wameuawa katika ufyatulianaji wa risasi wakati wa mauaji yaliyotokea katika matukio mawili tofauti nchini Afrika Kusini.

Polisi imesema mauaji hayo yalikitokea usiku wa kuamkia Jumamosi katika mji wa Lusikisiki, jimbo la Western Cape

Taarifa ya polisi imesema wanawake kumi na wawili na mwanaume mmoja waliuawa katika nyumba moja na wanawake watatu na mwanamume mwengine waliuawa katika nyumba nyingine. Muathiriwa mwengine mmoja amelazwa hospitalini akiwa kati hali mbaya.

Afrika Kusini ni moja ya nchi zenye viwango vya juu zaidi vya mauaji duniani. Na visa vya mauaji ya watu wengi vimeongezeka katika miaka ya hivi karibuni. Huku wakati mwingine watu hulengwa wakiwa nyumbani mwao.

Comments

Popular posts from this blog

TAZAMA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024.

WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2025 MAJINA HAYA HAPA.