Tume huru ya uchaguzi yabaini watu kujiandikisha zaidi ya mara moja
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema imebaini uwepo wa changamoto kwa baadhi ya watu kujiandikisha zaidi ya mara moja katika vituo tofauti wakati wa zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura mkoani Dar es Salaam. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani, huku akibainisha hatua ambazo zinachukuliwa na tume hiyo baada ya zoezi la uandikishaji kukamilika. Amesema baada ya zoezi la uandikishaji kukamilika katika vituo, tume inachakata taarifa za watu wote walioandikishwa kupitia mfumo maalum wa alama za vidole ambao una uwezo wa kuwabaini wapiga kura wote waliojiandikisha zaidi ya mara moja. “Kingine tume hufanya zoezi la kulinganisha sura za watu wote walioko kwenda daftari lengo ni kubaini iwapo kuna waliojiandikisha zaidi ya mara moja. “Pia iwapo itabainika mtu amejiandikisha zaidi ya mara moja, jina na taarifa za mtu huyo, hufutwa na mfumo katika vituo vingine na kubakizwa katika kituo cha mwisho alichojiandikisha ...












Comments
Post a Comment