Iran inataka kumuua Trump - Idara ya Ujasusi Marekani

 


25 Septemba 2024

Idara ya Ujasusi ya Marekani imemuonya mgombea urais kwa tiketi ya Republican, Donald Trump, juu ya kile inachodai ni kitisho cha kweli na cha wazi kutoka Iran inayotaka kumuua.

Mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Donald Trump.
Mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Donald Trump.Brandon/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa timu hiyo, idara ya ujasusi inaamini kumekuwa matukio ya mashambulizi dhidi ya Trump katika miezi ya karibuni na kwamba imeimarisha ulinzi kwa bilionea huyo anayetaka kurejea madarakani kupitia uchaguzi wa mwezi Novemba mwaka huu. Iran inakanusha vikali tuhuma hizo.


Marekani inafanya uchaguzi wake mkuu tarehe 5 Novemba, ambapo hadi sasa utafiti wa maoni ya wapigakura yanaonesha kuwa Trump na hasimu wake wa Democrat, Kamala Harris, wanachuana vikali.

CHANZO:DWSWAHILI

Comments

Popular posts from this blog

WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2025 MAJINA HAYA HAPA.

TAZAMA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024.