Posts

Showing posts from April, 2025

Kiongozi Mbio za Mwenge asisitiza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Image
  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ussi, ametoa wito kwa wananchi kuendeleza amani na utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Ussi aliyasema hayo alipokuwa akizungumza katika Wilaya ya Rufiji wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru kwa ajili ya kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kusambaza ujumbe wa kitaifa wa Mbio hizo. Aliwahimiza wananchi kuzingatia ujumbe wa mwaka huu unaosema: “Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani na utulivu,” akisisitiza kuwa uchaguzi uwe huru, wa haki na wa kumalizika kwa amani kama ilivyopangwa na taifa. Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Rufiji, Mohamed Mchengerwa, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), alisema kuwa mbio za Mwenge wa Uhuru zimekuwa chachu ya maendeleo nchini kwa kufika katika kila pembe ya Tanzania kukagua na kuchochea utekelezaji wa miradi inayogusa maisha ya wananchi. “Tu...

Geofrey Kiliba, rais mpya wa TAHLISO

Image
  Geofrey Kiliba, mwanafunzi wa Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (DIT), ametangazwa rasmi kuwa Rais mpya wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) kwa mwaka wa uongozi 2025/2026, katika uchaguzi mkuu uliofanyika leo visiwani Zanzibar. Kiliba alipata ushindi huo mkubwa kwa kuungwa mkono na kura nyingi kutoka kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TAHLISO, ambao wanawakilisha serikali za wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya elimu ya juu nchini. Akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi, Kiliba aliwashukuru wajumbe kwa imani waliyoionesha kwake, na kuahidi kuwa kiongozi mwenye maadili, uwazi, ushirikiano na weledi katika kutekeleza majukumu yake. Aliahidi kujenga TAHLISO imara, yenye kusikiliza na kutetea maslahi ya wanafunzi kwa nguvu na hekima. “Nitakuwa kiongozi mwenye masikio makubwa na mdomo mdogo; niko tayari kusikiliza hoja na haja zenu. Sote tuna ndoto za kuwa viongozi, lakini leo naomba mtangulize maono ili nitimize ya kwetu sote,” alisema Kiliba kwa u...

Watia nia CHADEMA 55, waibuka na hoja tisa kuhusu ‘no reforms no election’

Image
Picha: Mtandao Ofisi ya CHADEMA. Watia nia 55 wa ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa mwaka 2025, wakiwakilisha zaidi ya 200 walioonesha nia, akiwemo baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho, wameibuka na hoja tisa kuhusu msimamo wa chama huo wa kutoshiriki uchaguzi endapo hakutakuwa na mageuzi ya kisiasa ('No reforms, no election'). Kupitia waraka walioutuma Aprili 4, 2025 kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, watia nia hao wameeleza kuwa msimamo huo kwa sasa unakinzana na malengo yake ya awali. Wamedai kuwa haiwezekani kuzuia uchaguzi kwa kuwa nje ya mchakato huo, wakisema hatua hiyo inaweza kuchukuliwa kama kitendo cha jinai. Kwa mujibu wa waraka huo, njia pekee ya kuzuia uchaguzi isiyo huru ni kushiriki mchakato huo kwa kuingiza wagombea, ambao wanaweza kuhamasisha na kuongoza wananchi kuzuia uchaguzi katika maeneo mahsusi yenye viashiria vya hujuma, badala ya kuwa nje ya mchakato mzima. Hoja tisa kuu zilizowasilishwa: 1. ✍🏿 Mbinu ya Kuzuia Uchaguzi Kutoka ...

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi yatangaza nafasi za kazi za watendaji wa uchaguzi Tanzania Zanzibar

Image
  Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza nafasi za kazi za mratibu wa uchaguzi, msimamizi wa uchaguzi na msimamizi msaidizi wa uchuguzi ngazi ya jimbo watakaosimamia Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano na Madiwani kwa Tanzania Bara kwa upande wa Tanzania Zanzibar Kwa mujibu wa tangazo la Tume lililosainiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw. Kailima, R. K, nafasi hizo ni kwa Unguja na Pemba na wanaotakiwa kuomba nafasi hizo ni raia wa Tanzania, watumishi wa umma na sifa nyingine zilizoainishwa kulingana na nafasi inayoombwa. Tangazo hilo limemtaka kila mwaombaji aainishe nafasi anayoiomba, akitaja wilaya au jimbo analotaka kufanyia kazi na aambatishe vyeti vya elimu pamoja na maelezo binafsi (CV) na maombi yatapokelewa kuanzia tarehe 3 Aprili, 2025 hadi tarehe 23 Aprili, 2025 saa 9:30 Alasiri. Maombi hayo yanatakiwa kuwasilishwa katika Ofisi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi zilizopo Maisara kwa upande wa Unguja na Chakechake (Mtaa wa Miembeni) kwa upande wa Pemba kwa a...