Posts

Showing posts from February, 2025

FIFA yaifungia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC)

Image
 S hirikisho la soka Duniani FIFA limetangaza rasmi kuifungia Congo DR uanachama wake kwa muda usijulikana kutokana na machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini humo na kusababisha vifo. Kwa maana hiyo Congo DR timu yao ya Taifa, Vilabu vyao na Viongozi wao hawataruhusiwa kushiriki michezo yoyote ya Kimataifa (CHAN, AFCON, CAFCL, CAFCC, Kombe la Dunia) hadi adhabu hiyo itakapoondolewa.   Reactions:

TRA yamwaga nafasi za ajira 1,596

Image
  Dar es Salaam.  Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza nafasi 1,596 za ajira katika kada mbalimbali. Tangazo la nafasi hizo limetolewa leo Alhamisi Februari 6, 2025 na kusainiwa na Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo. “TRA inapenda kuajiri watumishi wenye sifa, uwezo na maadili kushika nafasi za kazi katika Idara ya Mapato ya Ndani, Forodha na Ushuru, Usimamizi na Utawala wa Rasilimali Watu, Huduma za Sheria, Menejimenti ya Manunuzi, Utafiti na Mipango, Fedha, Ukaguzi wa Ndani, Mambo ya Ndani na Idara ya Vihatarishi na Uzingatiaji. Kwa hiyo maombi yanaalikwa kutoka kwa Watanzania wenye sifa,”imeeleza taarifa hiyo. Aidha taarifa hiyo imeeleza maombi yote yafanywe kupitia mfumo maalimu wa ajira wa TRA ambao ni: https://recruitment.tra.go.tz/tra careers/User/UserHome.aspx. Kada zilizotangazwa nafasi TRA katika tangazo lake imeeleza nafasi hizo zipo katika kada zifuatazo: Ofisa Msimamizi Ushuru daraja la II (573), Ofisa Forodha daraja la II (232), Msaidizi wa Usimamizi wa Ushuru ...

Majina waliochaguliwa kujiunga Idara ya Uhamiaji haya hapa

Image
  Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo hayo limetolewa leo Alhamisi Februari 6, 2025 na Kamishna Jenerali wa idara hiyo. “Kamishna Jenerali wa Uhamiaji anawatangazia vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na Idara ya Uhamiaji kuripoti Chuo cha Uhamiaji cha Raphael Kubaga kilichopo Boma Kichakamiba, Wilaya ya Mkinga - Mkoani Tanga, Jumamosi Machi mosi 2025 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana,” imeeleza taarifa hiyo. Tazama hapa majina waliochaguliwa kujiunga na Idara ya Uhamiaji Pia, kwa walioomba na kuchaguliwa kupitia Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, wanatakiwa kuripoti Afisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Unguja (Tunguu) Jumatatu Februari 24, 2025 saa 2:00 asubuhi. Katika taarifa hiyo vijjana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo hayo wametakiwa kuripoti wakiwa na vyeti halisi vya elimu na fani mbalimbali. “Vyeti na nyaraka zinazotakiwa ni kama ifuatavyo: Cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha Taifa (Nida) au Namba ya Nida, vyeti halisi vya elimu ya kidato cha nne, cha sita na shahada na...

DRC yaingia mtegoni, M23 yaanzisha mashambulizi mapya yatwaa mji wa madini

Image
Siku moja baada M23 kudhaniwa kuanza kutekeleza sitisho la vita kufuatilia taarifa ya awali, suala hilo limeoneka kuwa ni mtego dhidi ya Majeshi ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Hii ni baada ya M23 kufanya shambulizi la kushtukiza na kuchukua Mji wa madini katika jimbo la Kivu Kusini, wakati wakiendelea kusonga mbele kuelekea mji mkuu wa Bukavu. Baada ya M23 inayotajwa kusaidiwa na Majeshi ya Rwanda kuuchukua mji wa kimkakati wa Goma  huko  Kivu Kaskazini, walitangaza kusitisha mapigano kwa ajili ya misaada ya kibinadamu kuanza siku ya Jumanne.  Hata hivyo sitisho hilo limeoneka kuwa mtego kwa DRC kutokana na mapigano makali yaliyoanza Februari 5, 2025 na kundi hilo likitajwa kuwa na washirika wake Wanyarwanda hii ni kwa mujibu wa shirika la habari la AFP.  M23 na majeshi ya Rwanda wameuchukua  mji wenye madini wa Nyabibwe, kilometa 100 kutoka  Bukavu na kilometa 70 kutoka uwanja wa ndege wa jimbo hilo. Kuanzishwa kwa mashambulizi hayo mapya mash...

KESI MAUAJI KATIBU CCM IRINGA: Mahakama yaahirisha hadi Feb. 17 kusubiri upelelezi

Image
MAHAKAMA ya Wilaya ya Iringa imeahirisha kesi ya mauaji ya aliyekuwa Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilolo, Christina Kibiki hadi Februari 17 itakapotajwa tena kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika   Akiomba kuahirishwa kwa kesi hiyo juzi, Wakili wa Serikali, Atupele Makoga, alisema kuwa wanaomba kesi hiyo ipangwe siku nyingine ili waweze kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo. Wakili wa utetezi, Barnabas Nyalusi kutoka kampuni ya mawakili ya BLS Attorney &Partner, aliiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Iringa, kuwahimiza upande wa Jamhuri kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo kutokana na siku 90 walizopewa kisheria kukabia kuisha. Wakili Nyalusi alidai mbele ya mahakama kuwa kesi hiyo inasikilizwa na kufuatiliwa na jamii kwa ukaribu na kwamba ni vema mchakato wa upelezi ukakamilika haraka ili ianze kusikilizwa. Kutokana na maombi hayo ya upande wa Jamhuri, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Iringa, Adelina Ngwaya, aliahirisha kesi hiyo...

Kocha Singida BS avutwa Yanga kumrithi Ramovic

Image
Muda mfupi baada ya kocha Sead Ramovic kubwaga manyanga, Yanga leo, Februari 4, 2025 imetangaza kumchukua kocha wa Singida Black Stars, Hamdi Miloud kuziba pengo lililoachwa na Mjerumani huyo. Taarifa iliyotolewa na Yanga imesema kuwa Ramovic ameondoka sambamba na msaidizi wake Mustafa Kodro. “Uongozi wa Klabu ya Young Africans SC umefikia makubaliano ya pande mbili kuvunja mkataba na Kocha Sead Ramovic na msaidizi wake Mustafa Kodro.   “Katika hatua nyingine, Klabu ya Young Africans SC inamtangaza Kocha wake mpya, Miloud Hamdi mwenye uraia wa Algeria na Ufaransa. “Kocha Hamdi mwenye uzoefu mkubwa wa kufundisha soka akiwa amefanya kazi barani Ulaya, Asia na Afrika, anaungana na timu mara moja kuanza majukumu yake mapya. “Kocha huyo mbali na uzoefu alionao, pia ana mafanikio makubwa katika soka la Afrika akishinda taji la Ligi Kuu ya Algeria na kucheza Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2015-2016 akiwa na USM Alger,” imefafanua taarifa hiyo ya Yanga. Miloud anajiunga na Yan...

Kagame: Rwanda itafanya lolote kujilinda, M23 wadaiwa kusitisha mapigano

Image
  Wakati Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ikiapa kuurejesha Mji wa Goma, jiji lenye takriban watu milioni 3, kutoka mikononi mwa waasi wa M23, imeendelea kuishutumu Rwanda kwa madai ya kutuma wanajeshi huko kuwaunga mkono waasi hao. Hata hivyo, katika mahojiano maalumu na CNN, Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ambaye amekanusha mara kadhaa tuhuma hizo, alisema hajui kama wanajeshi wa nchi yake wako mashariki mwa Kongo ambako mapigano kati ya kundi la M23 na vikosi vya Kongo yanaendelea. Kagame alisisitiza kuwa Rwanda itafanya kila linalowezekana kujilinda, huku akiishutumu Afrika Kusini kwa madai ya kutuma wanajeshi wake mashariki mwa DRC kwa lengo la kutafuta madini. Katika hatua nyingine, Muungano wa waasi wa Alliance Fleuve Congo (AFC), unaojumuisha waasi wa M23, umetangaza kusitisha mapigano kuanzia leo Februari 4. Taarifa inayodaiwa kuwa ya kundi hilo, iliyosambaa kwenye mtandao wa X (Twitter), ilieleza kuwa usitishaji huo wa mapigano umefanyika kwa sababu za kibi...

Chama cha Walimu Tanzania watangaza nafasi za Kazi

Image
  Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ndicho chama rasmi cha wafanyakazi kinachowakilisha walimu Tanzania Bara.   CWT iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini namba 6 ya 2004, imejitolea kuboresha mazingira ya kazi, kutetea haki za walimu, na kuhakikisha huduma za ubora wa juu kwa wanachama wake.  Ili kuimarisha utoaji huduma, CWT inaajiri nafasi nyingi katika makao makuu yake mjini Dodoma. Ikiwa una sifa zinazohitajika na una shauku ya kufanya kazi katika mazingira yenye nguvu, hii ni fursa yako! <<<<<<<<<BOFYA HAPA KUONA TANGAZO HILO>>>>>>>>

Fedha Alizowekewa Mzize na Timu ya Al Ittihad hizi hapa

Image
  Klabu ya Al Ittihad ya ligi kuu soka nchini Liby imetenga ada ya uhamisho ya zaidi ya TSh bilioni 3 kwaajili kumnasa mshambuliaji wa klabu ya Yanga Clement Mzize ambaye amewaka sana kwa siku za karibuni. Al Ittihad mbali na fungu hilo la uhamisho wamemuwekea mezani Mzize ada binafsi ya kusaini mkataba (sign-on fee) ni zaidi ya TSh bilioni 1.3 na mshahara wa Tsh Milioni 50 kwa mwezi huku wakimshawishi kusaini mktaba wa miaka miwili kinda huyo wa zamani wa timu za vijana za Yanga. Wakati hayo yakiendelea nje ya uwanja, Mzize ndiyo kwanza ananogesha biashara na kuwapa presha waarabu hao baada ya jana kufunga goli moja kati ya manne waliyoshinda dhidi ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara

Diamond Platnumz – Nitafanyaje (Official Music Video)

Image
Diamond Platnumz – Nitafanyaje (Official Music Video) SUPASTAA wa Bongo Fleva na CEO wa Lebo ya WCB, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, ametoa video ya wimbo wake mpya unaoitwa Nitafanyaje. chanzo:Globalpublishers

MAJINA AJIRA MPYA SERIKALINI HAYA HAPA, WALIMU 'KIBAO'

Image
  Walimu hao wamepangiwa katika halmashauri tatu kama ifuatavyo; Halmashauri ya Manispaa Temeke (74), Halmashauri ya Mji Kibaha (9) na Halmashauri ya Manispaa Kinondoni (57). Upande wa kada zao, walimu hao wapya walioajiriwa ni kama ifuatavyo: Mwalimu daraja la III B fizikia (14), mwalimu daraja la III B - hisabati (27), mwalimu daraja la III B  biashara (4), mwalimu daraja la III C fizikia (8), mwalimu daraja la III C hisabati (28). Kada nyingine ni: Mwalimu daraja la III C sanaa (2) na mwalimu daraja la III C biashara (12). Taarifa hiyo imeeleza kuwa: “Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kati ya Agosti 14, 2024 na Januari 17, 2025 kuwa matokeo ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyoorodheshwa katika tangazo hili. >>>>>>>BOFYA HAPA KUONA MAJINA HAYO<<<<<<< <<<<<<<<<<BOFYA HAPA KUONA MAJINA 2>...

HILI HAPA CHIMBUKO LA M 23

Image
  Chanzo cha picha, AFP Maelezo kuhusu taarifa Author, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kumeshuhudiwa mzozo na ukosefu wa utulivu …Kwa muda usiokuwa chini ya miongo mitatu. Ila katika muongo mmoja uliopita, mapigano makali yamezuka mara kwa mara. Japo eneo hilo linalojumuisha majimbo ya Ituri, Kivu kusini na Kivu Kaskazini yana jumla ya makundi ya wapiganaji zaidi ya 129, kundi la waasi la M23, ambalo ndilo kuu lililobuniwa baada ya makubaliano ya Machi 23 ya kutafuta amani imekuwa na historia ya machafuko. Pamoja na sababu za kihistoria, mashindano ya kikanda, na machafuko ya ndani, hali hiyo kwa mara nyingine tena inavuta hisia za kikanda na za kimataifa. Chanzo cha picha, AFP Kundi la M23 ni nini na lilianza vipi? Huwezi kuzungumzia M23 bila kuangazia historia ya jamii ya Watutsi katika eneo la mashairiki mwa Kongo, na ambao pia wako nchini Rwanda. Makundi mbalimbali yalibuniwa ili kutetea maslahi ya jamii ya watutsi katika eneo hilo. Mwaka 2006 CNDP (National...