Posts

Mtoto wa Osama Bin Laden atakiwa kuondoka nchini Ufaransa

Image
  Serikali ya Ufaransa imemuamuru Omar bin Laden, mtoto wa kiongozi aliyeuawa wa Al Qaeda Osama bin Laden, kuondoka nchini humo kutokana na machapisho yake kwenye mitandao ya kijamii. Waziri mpya wa mambo ya ndani wa Ufaransa Bruno Retailleau, ameandika kwenye mtandao wa X kwamba mtoto huyo wa  Bin Laden  alichapisha mwaka jana maoni kwenye mitandao yake ya kijamii ambayo yalitetea vitendo vya ugaidi.Omar mwenye umri wa miaka 43, alizaliwa na kuishi nchini Saudi Arabia kabla ya kuelekea katika mataifa ya Sudan na Afghanistan. Alijitenga na baba yake akiwa na umri wa miaka 19 na akaamua kuishi na mke wake raia wa Uingereza huko Normandy kaskazini mwa Ufaransa mnamo mwaka 2016 akijishughulisha pia na uchoraji. Swahili.

BUNGE LA KENYA LAMUONDOA MADARAKANI Naibu Rais.GACHAGUA

Image
  HATIMAYE Bunge la Kenya,limemuondoa madarakani Naibu Rais wa Kenya,Rigathi Gachagua, kutokana na mashtaka 11 yaliyokuwa yanamkabili ikiwamo la ufisadi na kuendeleza ukabila akiwa ni kiongozi wa Serikali. Mashtaka mengine ni pamoja ukiukaji wa Katiba ya Kenya,kutokumheshimu Rais na kwenda kinyume na Sera za Serikali. Bunge hilo la Kitaifa la Kenya limeidhinisha Gachagua kuondolewa madarakani baada ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye. Katika kura zilizopigwa kuamua hatma yake, wabunge 281 waliunga mkono hoja ya kumuondoa kiongozi huyo madarakani, huku wabunge 44 wakipiga kura ya kupinga na mbunge mmoja akikataa kupiga kura. Awali kabla ya kura hizo, kupigwa Naibu Rais hiyo, aliweka matumaini yake kwa Wabunge waliojiandaa kupiga kura kuhusu hoja yake ya kuondolewa madarakani. Gachagua alisema anaheshimu na anaamini Bunge litafanya uamuzi sahihi. Naibu huyo, alikuwa akiwahutubia wabunge alipofika mbele ya Bunge kujibu tuhuma zilizowasilishwa kwenye hoja yake ya kuondolewa mada...

Hoja Ya Kumuondoa Madarakani Naibu Wa Rais Wa Kenya Yaanza Kujadiliwa Bungeni

Image
  BUNGE la Kitaifa nchini Kenya leo Oktoba 8, 2024 limeanza kujadili hoja ya kuondolewa madarakani kwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua. Hatua hii ni baada ya Mbunge wa Kibwezi Magharibi Mwengi Mutuse kuwasilisha sababu 11 kupitia hoja ya kutaka kumuondoa madarakani mnamo tarehe Septemba 26, 2024. Naibu Rais wa Kenya Geoffrey Rigathi Gachagua anatarajiwa kufika mbele ya Bunge la kitaifa mwendo wa saa kumi na moja jioni ya Jumanne Octoa 8 ili kujitetea dhidi ya mashtaka 11 yaliyowasilishwa. Baada ya saa mbili za kujieleza na kujibu maswali, Gachagua ataondoka bungeni na kuwaacha wabunge wakijadili majibu yake, kwa muda. Usiku wa leo, Spika Wetangula anatarajiwa kutangaza rasmi kwamba kikao maalum cha bunge kiko tayari kupigia kura hoja hiyo ya kumuondoa kazini Naibu Rais Gachagua. Atawaomba viranja wa bunge kupiga kengele ya kuidhinisha kura hiyo kupigwa. Kura huweza kupigwa kwa njia ya siri kupitia mashine za Kompyuta wanapoketi Bungeni. Kila mbunge ana kadi maalum yenye taarifa zae ...

Mh.Diwani afariki dunia

Image
  DIWANI wa Kata ya Itwangi Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Sonya Mhela amefariki dunia, akipatiwa matibabu Bugando Jijini Mwanza. Taarifa za msiba huo zilitolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Ngassa Mboje ambaye amesema wiki iliyopita Sonya alipata ajali ya pikipiki akavunjika mguu.  Amesema baada ya kupata matibabu ya awali alihamishiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza, lakini wakati akiendelea na matibabu hali yake ilibadilika na kufariki dunia. Mazishi ya diwani huyo yamefanyika jana Oktoba 7,2024 nyumbani kwake Itwangi. Nipashe.

Jacob apata dhamana atoa mambo matano mazito

Image
Home Habari Biashara Michezo Burudani Makala Safu Maoni Maktaba EDITIONS The Guardian Nipashe Nipashe Ju ALIYEKUWA Meya wa Kinondoni na Ubungo, Boniface Jacob, maarufu kwa jina la ‘Boni Yai' ametaja mambo matano aliyojifunza akiwa mahabusu atakayokwenda kuyasimamia baada ya kutangazwa mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani. Akizungumza jana katika viunga vya Mahakama ya Kisutu baada ya kupata dhamana hiyo, alisema kukaa kwake gerezani kumemsaidia kuifahamu nchi, kwa kuwa alikutana na wafungwa waliomweleza matatizo yao. Alisisitiza uzoefu alioupata anataka kuutumia katika kuendeleza mapambano yake kudai haki kwa Watanzania, hasa waliokosa fursa za kisheria. Alisema kutokana na funzo alililopata atawalipia  wafungwa 10 faini wanazodaiwa katika Gereza la Segerea,  huku mmoja akiwa tayari amelipiwa faini  na wengine tisa wakikamilishiwa leo ili wawe huru. Pia, aliahidi kuwatafutia mawakili na kulipa gharama, wafungwa 20 wa makosa mbalimbali, mengine yakiwa ...

Boni Yai aachiwa kwa dhamana

Image
Home Habari Biashara Michezo Burudani Makala Safu Maoni Maktaba EDITIONS The Guardian Nipashe Nipashe Jumapili ALIYEKUWA Meya wa Manispaa ya Ubungo, Dar es Salaam Boniface Jacob maarufu kama 'Boni Yai' amepata dhamana, baada ya Hakimu Mkazi Kisutu, kutupilia mbali pingamizi lililowasilishwa na upande wa Jamhuri kupinga dhamana ya kada huyo. Jacob amepata dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wenye barua za Serikali za Mitaa na kusaini bondi ya sh milioni saba na pia ametakiwa asitoke nje ya nchi bila kibali cha Mahakama. Uamuzi huo mdogo, umetolewa leo Oktoba 7,2024 na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Franco Kiswaga alisema kuwa kiapo cha RCO wa Mkoa wa Polisi Kinondoni, Davis Msangi hayana maelezo yaziada ya kutosha kuzuia dhamana hiyo ya Jacob. Alisema sababu zilizotolewa hazina maelezo ya ziada ya kwanini mahakama isitoe dhamana, kwamba iwapo mjibu maombi ametoa maelezo juu ya usalama wake alitegemea muombaji (Jamhuri) kupeleka uthibitisho juu ya...